Publisher's Synopsis
Baada ya kufanya vizuri katika mtihani, Sudi na Shada wanapelekwa na
wazazi wao kwenye mbuga ya wanyama. Wanapofika mbugani, Sudi
anatoweka pasi na yeyote kumwona. Wazazi wake na dada yake
wanaanza kumtafuta. Je, Sudi anapatikana?
Hadithi Mufti za Longhorn ni mfululizo mpya wa hadithi ambazo
zimeandikwa kulingana na mtaala mpya. Hizi hadithi zinalenga kukuza
ujuzi wa wanafunzi kupitia kwa uvumbuzi wa maarifa na zinaimarisha
uelewa wao wa masuala ibuka katika jamii. Hadithi hizi sio tu za kuelimisha
na kuburudisha, bali pia zimeambatanishwa na mazoezi ambayo
yatawasaidia wanafunzi kuimarika kiubunifu, kimawazo na kifikra.